Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile amefanya ziara ya kutembelea Shirika la Reli Tanzania(TRC) Kwa ajili ya kujifunza na kujionea miradi inayoendelea chini ya Usimamizi wa Shirika Hilo na kukagua Stesheni ya treni ya kisasa ya SGR ya Tanzanite Jijini Dar es salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe katika Bandari ya Kilwa Masoko leo 18 Septemba 2023
Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara akizungumza na Waziri wa Wizara hiyo, Profesa Makame Mbarawa mara baada ya Waziri huyo kuwasili Mkoani Mtwara leo.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa akizungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara mara baada ya Waziri huyo kuwasili Mkoani Mtwara.
Aliyekuwa Katibu Mkuu-Uchukuzi, Gabriel Migire (kushoto) akimkabidhi rasmi ofisi Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara mara baada ya kusaini nyaraka za makabidhiano katika ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara (kulia) na aliyekuwa Katibu Mkuu-Uchukuzi, Gabriel Migire (kushoto), wakisania nyaraka za makabidhiano katika ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam.
Hafla ya makabidhiano ya Makasha 5 ya ubaridi kati ya Shirika la Mpango wa chakula Duniani (WFP) na Wizara ya Uchukuzi kupitia Shirika la Reli Tanzania(TRC) yaliyofanyika kwenye eneo la upakiaji na upakuaji wa bidhaa la TRC lililopo Ilala Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Uchukuzi, Pro. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Godius Kahyarara mara baada ya Waziri huyo kuzindua bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (wa pili kulia) akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC), Ally Amani (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti, Ofisi ya Msajili wa Hazina, Neema Musomba (kulia) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Amina Lumuli wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa bodi ya TRC, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa Mwenyekiti na Wajumbe wa Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) hawapo pichani wakati alipozindua bodi hiyo, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng.Mohamed Besta alipowasili katika Hafla ya Kumkabidhi Mkandarasi Henan Highway Engineering Group kujenga barabara ya Sabasaba-Sepuka-Ndago-Kizaga (KM 77.6) mkoani Singida.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa akizungumza na Wananchi wa Iramba wakati wa Hafla ya Kumkabidhi Mkandarasi Henan Highway Engineering Group kujenga barabara ya Sabasaba-Sepuka-Ndago-Kizaga (KM 77.6) mkoani Singida.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Bw. Ludovick Nduhiye akiwa Menejimenti na Wakuu wa Taasisi zilizochini ya Wizara ya Ujenzi katika hafla ya makabidhiano ya Ofisi kati ya Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa na Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa yaliyofanyika leo, Septemba 08, 2023 Jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa (katikati) akizungumza Menejimenti ya Wizara na Wakuu wa Taasisi zilizochini ya Wizara ya Ujenzi mara baada ya kukabidhiwa ofisi na Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (kulia) leo, Septemba 08, 2023 Jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya.
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (katikati) akizungumza Menejimenti ya Wizara na Wakuu wa Taasisi zilizochini ya Wizara ya Ujenzi mara baada ya kukabidhi ofisi kwa Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa (kushoto) leo, Septemba 08, 2023 Jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa akipokea vitendea kazi kutoka kwa aliyekuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa ambaye sasa ni Waziri wa Uchukuzi wakati wa makabidhiano ya ofisi yaliyofanyika leo, Septemba 08, 2023 Jijini Dodoma.
Kushoto ni Katibu Mkuu wa Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Ally Possi wakifuatilia majadiliano yaliyofanyika kati ya Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarwa, Waziri wa Uchukuzi na Lojistiki wa Zambia Frank Tayali, Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Chen Mingjian (hawapo pichani) kwa njia ya mtandao kuhusu kuboresha utendaji na Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA).
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa akifuatilia majadiliano yaliyofanyika kati yake na Waziri wa Uchukuzi na Lojistiki wa Zambia Frank Tayali, Balozi wa China Nchini Tanzanai, Mhe. Chen Mingjian kwa njia ya matandao kuhusu kuboresha utendaji na Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA).
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa akifuatilia majadiliano yaliyofanyika kati yake na Waziri wa Uchukuzi na Lojistiki wa Zambia Frank Tayali, Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Chen Mingjian kwa njia ya matandao kuhusu kuboresha utendaji na Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent L. Bashungwa (Kushoto) akitoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Daud Kondoro (kulia) wakati wa ziara yake ya Kukutana na Menejimenti ya TBA, tarehe 07 Septemba 2023 jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent L. Bashungwa (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour wakati akiwasili Makao makuu ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa ajili ya kukutana na kuzungumza na Menejimenti ya TBA ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi, Leo tarehe 07 Septemba 2023 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya ujenzi Mha, Balozi Aisha Amour, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa (katikati) wakati alipotembelea ofisi za wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), jijini Dodoma
Waziri wa Ujenzi, Mhe Innocent Bashungwa, akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mha ,Balozi Aisha Amour ,wakati alipotembelea ofisi za Wakala wa Ufundi na Umeme Jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akijibu maswali ya wabunge katika Bunge la 12, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akifafanua jambo kwa menejimenti ya Wizara hiyo, mara baada ya kupokelewa na kukaribishwa katika ofisi za Wizara hiyo, jijini Dodoma tarehe 04 Septemba, 2023.