Makatibu Wakuu, Manaibu Makatibu Wakuu na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, wakifuatilia bajeti ya Wizara yao iliyowasilishwa Bungeni leo na Waziri Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani).
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Atupele Mwakibete wakiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Bw. Giliard Ngewe na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dakta, Agnes Kijazi Bungeni mjini Dodoma.
Katibu Mkuu (Ujenzi), Balozi, Eng. Aisha Amour (kushoto), akiteta jambo na Mbunge wa Mufindi Kusini Mhe. David Kihenzile mara baada ya kukamilika kwa kikao cha Bunge jijini Dodoma, (wa pili kushoto), ni Naibu Katibu Mkuu Ujenzi Bw. Ludovick Nduhiye akifuatilia.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akiwasilisha hoja Bungeni leo, jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakuu wa Taasisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, wakiingia Bungeni.
Ujenzi wa Daraja jipya la Wami lenye urefu wa mita 513.5 ukiendelea, mkoani Pwani.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Nyahua – Chaya (Km 85.4), mkoani Tabora.
Watumishi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika ufunguzi wa barabara ya Tabora – Nyahua (Km 85.4), uliofanyika tarehe 17/05/2022, eneo la Tura mkoani Tabora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED), Waleed SH. Albahar wakitoa kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa barabara ya Nyahua – Chaya (Km 85.4) katika kijiji cha Tura, mkoani Tabora. Wengine katika picha ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa.
Muonekano wa sehemu ya barabara ya Tabora - Koga - Mpanda, mkoani Tabora.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiteta jambo na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, katika ufunguzi wa barabara ya Tabora - Koga - Mpanda (Km 342.9) kwa kiwango cha lami, mkoani Tabora.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, akiwasikiliza wataalam wa mizani kutoka nchini Ufaransa, waliofika Ofisini kwake jijini Dodoma, kujadili masuala mbalimbali ikiwemo uwekaji wa mifumo ya kisasa ya kudhibiti uzito wa magari katika mizani nchini.
Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi Hussein Kattanga (katikati) akimsikiliza Katibu Mkuu-Uchukuzi, Gabriel Migire (kulia), kuhusu maendeleo ya mradi wa bandari kavu ya Kwala, wakati Katibu Mkuu Kiongozi alipotembelea mradi huo Mkoani Pwani 16 Mei 2022.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani), mkoani Tabora.
Naibu Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Bw. Ludovick Nduhiye, akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Sekta ya Ujenzi, mkoani Tabora. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Burian na Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bw. Eric Lengama.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Burian, Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Balozi, Eng. Aisha Amour, pamoja na viongozi wengine wa Baraza la Wafanyakazi wakiimba wimbo wa mshikamano katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi, Balozi, Eng. Aisha Amour, akizungumza mbele ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa, ambaye ni mgeni rasmi mara baada ya kufungua kikao cha Baraza la Wafanayakazi lililofanyika mkoani Tabora.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akisisitiza jambo kwa wataalamu wa BRELA, alipokagua banda lao kabla ya kufunga mkutano wa siku mbili wa mwaka wa makandarasi, jijini Dodoma.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao kati yake na Balozi wa Korea Kusini Nchini, Kim Sun Pyo (kulia) kwenye ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Mei 14, 2021. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi, Eng. Aisha Amour, akisalimiana na Msajili wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Rhoben Nkori, katika mkutano wa mwaka wa mashauriano wa Bodi hiyo uliowakutanisha makandarasi na wadau wa Sekta ya Ujenzi, jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, akipata maelezo katika Banda la Brela wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa mashauriano uliofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (wa pili kushoto), sehemu ya Mawaziri na Wakuu wa Taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta Binafsi kutoka Nchini Tanzania wakiwa katika Mkutano wa Biashara wa Tanzania na Uganda uliofanyika 11 Mei 2022, nchini Uganda.
Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Godfrey Kasekenya akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti (hawapo pichani), katika kikao kazi kati ya Kamati hiyo na wataalam wa Wizara ya Ujenzi kilichofanyika jijini Dodoma.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa meli ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu kwenye Bandari ya Mwanza South jijini Mwanza, Mei 7, 2022. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara Ujenzi na Uchukuzi-Uchukuzi, Mhe. Atupele Mwakibete, bungeni jijini Dodoma, hivi karibuni.