16th JOINT TRANSPORT SECTOR REVIEW MEETING
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Mhe. David Kihenzile , akiwasilisha Taarifa ya Utendaji ya kampuni ya Huduma za Meli (MSCL), mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu (haipo pichani) kwa kipindi cha Julai – Oktoba, 2023 Bungeni, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe David kihenzile amekagua na kuridhishwa na maendeleo, usimamizi na maboresho yanayoendelea kwenye uwanja wa ndege wa Arusha ikiwemo jengo jipya la abiria na sehemu ya kuruka na kutua ndege.
Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na LATRA leo imeendesha Mkutano na Kupokea maoni ya wadau wa Usafiri wa Reli nchini kuhusu Rasimu za Kanuni Mpya za Sheria ya Reli za mwaka 2023 zitakazotumika kuruhusu Watoa huduma binafsi kutumia reli za TRC. Mkutano huu umefanyika katika ukumbi wa mkutano uliopo katika Chuo cha Utalii, Dar es Salaam Oktoba 16, 2023.
Waziri wa Uchukuzi Mhe. Profesa Makame Mbarawa (katikati) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi na Maendeleo ya Miundombinu Nchini Zimbabwe Mhe. Mha. Joy Makumbe (wa pili kushoto), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ofisi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Jijini Harare nchini Zimbabwe, tarehe 16 Oktoba, 2023. Wengine katika picha ni Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. Simon Sirro (kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mku wa TPA Mha. Juma Kijavara ( kulia).
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la huduma za Meli Tanzania (MSCL) Erick Hamisi (Kulia) na Mkurugenzi wa kampuni ya Dearsan Shipyard Murat Gordt (Kushoto) wakionyesha mikataba iliyosainiwa katika hafla iliyofanyika bandari ya Kigoma Mkoani Kigoma, ambapo miradi mitatu ilisainiwa ambayo ni mradi wa ujenzi wa kiwanda cha meli na ujenzi wa meli mbili za mizigo.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akizungumza na wananchi (hawapo pichani)katika hafla ya utiaji Saini mikataba mitatu ya ujenzi wa kiwanda cha meli na meli mbili za mizigo, hafla iliyofanyika katika bandari ya Kigoma Mkoani Kigoma.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akizungumza na menejimenti ya Shirika la Reli nchini (TRC) na kutoridhishwa na utendaji kazi wake hususan katika kusafirisha mizigo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt Ally Possi, akiongea na Uongozi pamoja na Kukagua na kutembelea Miradi mbali mbali ya maendeleo inayotekelezwa na kusimamiwana na Kampuni ya Huduma za Meli Nchini(MSCL), ikiwemo ukarabati wa Meli ya Mafuta ya MT SANGARA ambayo ukarabati wake umefikia asilimia 92 Mkoani Kigoma.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi David Kihenzile (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini (TAA) Mussa Mbura kuhusu maeneo ya biashara yaliyopo katika jengo la tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea jengo hilo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA) Mhandisi Rehema Myeya akimuonyesha Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi David Kihenzile maeneo mbalimbali ya Jengo la tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Julius Nyerere (JNIA) wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea jengo hilo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi David Kihenzile akizungumza na Menejimneti ya Mamlaka ya Viwanja cha Ndege Nchini (TAA) hawapo pichani, wakati alipokutana nao, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, David Kihenzile (katikati mstari wa kwanza) katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini (TAA), mara baada ya kuzungumza nao jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi David Kihenzile akimsikilza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vha Ndege Nchini (TAA) Mussa Mbura, wakati Naibu Waziri huyo alipokutana na kuzungumza na Menejimenti ya TAA, jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, David Kihenzile akimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Hali ya Hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA), Salama Said kuhusu namna taarifa za hali ya zinavyotafsiriwa wakati Naibu Waziri huyo alitembelea ofisi za Mamlaka hiyo, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, David Kihenzile akimsikiliza Msimamizi wa Kitengo cha Uchambuzi wa Hali ya hewa Kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA), Aboubakar Lungo kuhusu uchakataji wa taarifa za hali ya hewa, wakati Naibu Waaziri huyo alipotembelea ofisi za Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akimmkabidhi vitendea kazi mmoja wa wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini (TAA) Mhandisi Baraka Mwambage mara baada ya kuzindua bodi hiyo hawapo, jijini Dare es Salaam leo.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa katika picha ya pamoja na wajuumbe wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini (TAA) mara baada ua kuizindua, jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akizungumza na Wajumbe wa Bodi, Menejimenti na Watumishi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini (TAA) hawapo pichani, wakati alipozindua bodi ya TAA jijini Dodoma leo.
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na Waandishi wa Habari, mara baada ya kukagua Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha tatu Makutopora Mkoani Singida mpaka Tabora kilometa 368
Kazi ya Ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha tatu Makutopora Mkoani Singida mpaka Tabora kilometa 368 unaendelea.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dkt Ally Possi, akikagua utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya maendeleo inayosimamiwa na Kampuni ya Huduma za Meli Nchini(MSCL) iliyopo Jijini Mwanza
Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano wa Ushoroba wa Kati wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Tanzania, Prof. Godius Kahyarara (hayupo pichani) wakati wa kikao kilichofanyika kwa siku moja jijini Dar es Salaam. Ushoroba huo unajumuisha nchi za Rwanda, Uganda, Burundi, Malawi, Zambia, Tanzania na DRC.
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa akizungumza na Wataalam katika banda la Jeshi la Zimamoto wakati alipotembelea banda hilo katika maadhimisho ya siku ya Bahari Duniani yanayofanyika kitaifa katika Wilaya ya Chake chake, Mkoa wa Kusini Pemba.
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Usalama na Mazingira Wizara ya Uchukuzi Bi. Stela Katondo na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Wakala wa Meli Nchini (TASAC), Kapteni Mussa Manda baada ya Waziri huyo kufungua rasmi maadhimisho ya siku ya Bahari Duniani yaliyofanyika kitaifa katika Wilaya ya Chake chake , Mkoa wa Kusini Pemba.