Muonekano wa Daraja la Ruhuhu linalounganisha wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma na wilaya ya Ludewa mkoani Njombe, ambalo tayari limeshaanza kutumika.
Muonekano wa reli ya SGR na treni ya ufundi ambayo ujenzi wake unaendelea sehemu ya Isaka-Mwanza.
Baadhi ya Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Viongozi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), wakifatilia kwa makini taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kutoka kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Eng. Godfrey Kasekenya, wakati akiwasilisha kwa Kamati hiyo, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Sekta ya Ujenzi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, jijini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango akiweka simenti kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR, Sehemu ya Tabora hadi Isaka KM 165.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, akitoa maelekezo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo-Busisi), lenye urefu wa kilometa 3.2, jijini Mwanza. Ujenzi wa daraja hilo wafikia asilimia 63.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Eng. Godfrey Kasekenya, akikagua maandalizi ya ujenzi wa miundombinu ya Awamu ya Tatu ya Mabasi Yaendayo Haraka (BRT), itakayoanzia kutokea Jiji la Dar es Salaam kwenda Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere hadi Gongolamboto (KM 24
Sehemu ya Wajumbe wa Menejimenti na watumishi wa Uchukuzi, wakimsikiliza Kaimu Meneja wa Mradi wa MV. Mwanza Mhandisi Elias Kivara, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa meli hiyo wakati walipotembelea mradi huo hivi karibuni.
Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala-Ujenzi, Mrisho Mrisho akitoa salam za pole kwa wanafamilia (hawapo pichani) wa aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Barabara-Uchukuzi, Bw. Hassan Mabula jijini Mwanza hivi karibuni.
Sehemu ya Watumishi wa Uchukuzi, wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wa kituo cha kulelea Watoto cha Tanzania Children Rescue Centre-TCRC cha jijini Mwanza mara baada watumishi kula nao chakula cha mchana hivi karibuni.
Katibu Mkuu-Uchukuzi, Gabriel Migire akitoa salam za pole katika msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Barabara-Uchukuzi, Bw. Hassan Mabula uliotokea mwanzoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Watumishi wa Uchukuzi wakimsikiliza Katibu Mkuu-Uchukuzi, Gabriel Migire (hayupo pichani) wakati akitoa salam za pole kwa wanafamilia na watumishi wa sekta hiyo kwa msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Barabara-Uchukuzi, Bw. Hassan Mabula uliotokea mwanzoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu-Uchukuzi, Dkt. Ally Possi akitoa salam za pole katika msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Barabara-Uchukuzi, Bw. Hassan Mabula uliotokea mwanzoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akikagua ujenzi wa barabara za chini za watembea kwa miguu katika maeneo yenye msongamano mjini Kigoma na kutoa maelekezo kwa Mtendaji mkuu wa TANROADS Eng. Rogatus Mativila na Meneja wa TANROADS mkoa wa Kigoma Eng. Narcis Choma namna bora ya kuendeleza ujenzi huo.
Watendaji wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), wakifuatilia hafla ya kusaini mkataba wa ujenzi wa jengo la abiria na mnara wa kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Kigoma.
Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege QS. Mwanahamisi Kitogo (kulia), akifuatilia hotuba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani), wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa ujenzi wa jengo la abiria na mnara wa kuongozea ndege katika kiwanja cha ndege cha Kigoma.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa na Mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye, na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kigoma Bw, Jamal Tamim wakishuhudia utiaji saini mkataba wa ujenzi wa jengo la abiria, mnara wa kuongozea ndege na barabara za kuingia katika kiwanja cha ndege cha Kigoma.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa Mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila alipokagua moja ya daraja la ndani la watembea kwa miguu katika kijiji cha Makere wilayani Kasulu.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa na Mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye wakishuhudia utiaji saini wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami ya Kibondo-Mabamba Km 47.9, kati ya Mtendaji mkuu wa TANROADS na Mwakilishi wa Kampuni ya CHICO, mkoani Kigoma.
Muonekano wa barabara ya Nduta-Kibondo-Kabingo KM 62.5 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea mkoani Kigoma.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akikagua barabara ya juu katika makutano ya barabara ya Kilwa na Mandela kabla ya kuruhusu magari kuanza kupita eneo hilo katika makutano ya barabara ya Kilwa na Mandela jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa barabara ya juu katika makutano ya barabara ya Kilwa na Mandela jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Viongozi wa Serikali wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani) wakati wa hafla ya utiaji saini Mkataba wa ujenzi wa barabara ya Kitulo hadi Iniho KM 36.3 kwa kiwango cha Lami, iliyofanyika Wilayani Makete Mkoani Njombe.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mhandisi Rogatus Mativila akiwa na Muwakilishi wa Kampuni ya M/S China National Aero-Technology Engineering Corporation (wa pili kulia) wakionyesha mkataba wa Ujenzi wa Barabara ya Kitulo hadi Iniho KM 36.3 kwa kiwango cha Lami, mara baada ya kuusaini Wilayani Makete, Mkoani Njombe.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya mara baada ya kushuhudia hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa barabara ya Ibanda-Kajunjumele (KM 22), Kajunjumele hadi Kiwira Port (KM 6) na Kajunjumele hadi Itungi (KM 4), Uliosaniwa katika Viwanjavya shule ya Msingi Mpanda, wilayani Kyela, mkoani Mbeya.
Title | Tarehe | Pakua |
---|---|---|
TANGAZO LA KOZI MAALUM YA MAOPARETA WA MITAMBO YA KAZI ZA UJENZI (GRADER OPERATOR COURSE) | 2022-11-09 | Pakua |