Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof Makame Mbarawa akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe Selemani Kakoso na Wajumbe wa kamati hiyo (hawapo pichani), wakati walipotembelea na kukagua Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA).
Kichwa cha Treni ya kawaida-MGR cha kuvutia mabehewa ya abiria na mizigo kwa njia kuu aina ya 88 class kikifanyiwa ukarabati ndani ya Karakana ya Ukarabati wa Vichwa vya Treni ya kawaida-MGR Mkoani Morogoro
Kaimu Katibu Mkuu-Sekta ya Ujenzi, (wa tatu kulia mbele) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Sekta ya Ujenzi, mara baada ya kufungua semina ya mafunzo ya masuala ya afya, yaliyofanyika Jijini Dodoma.
Kaimu Katibu Mkuu-Sekta ya Ujenzi, Bi Saumu Mruke, akifanya vipimo vya afya kuhamasisha upimaji wa afya kwa hiyari kwa watumishi wa Sekta hiyo mara baada ya ufunguzi wa Semina ya Masuala ya afya kwa watumishi wa Sekta hiyo, jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Ludovick Nduhiye, akifafanua jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakati wakipokea taarifa ya Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT), mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete, akisisitiza jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakati wakipokea taarifa ya Taasisi ya Teknolojia ya Ujenzi (ICoT), mkoani Morogoro.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akimsikiliza Katibu Mkuu-Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour kuhusu utekelezaji wa maradi mbalimbali ya ujenzi wa barabara, wakati kamati hiyo ilipokagua barabara ya Njombe-Moronga KM 53.9 ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami umekamilika mkoani Njombe.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa katika picha ya pamoja na Waziri wa Miundombinu, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wa Nchini Zambia, Mhe. Mhandisi Charles Milupi (katikati), mara baada ya Waziri Prof. Mbarawa kuzungumza nae, mjini Lusaka.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete akifafanua jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu (hawapo pichani), wakati kamati hiyo ilipotembelea Mradi wa SGR Sehemu ya Morogoro-Makutupora.
Katibu Mkuu (Uchukuzi), Gabriel Migire, akimsikiliza Mhe. Lt. Jen. Mathew Mkingule, Balozi wa Tanzania nchini Zambia baada ya kuwasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kenneth Kaunda, Lusaka - Zambia kwa ajili ya kushiriki katika Kikao cha Bodi ya TAZARA.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa akipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Zambia Balozi Mhe. Lt. Jen. Mathew Mkingule, muda mfupi baada ya kuwasili katika Ofisi za TAZARA Jijini Lusaka, Zambia.
Naibu Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Ally Possi, akisisitiza jambo wakati wa kikao kilichowakutanisha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu pamoja na watendaji wa Wizara kujadili kuhusu Muundo na Majukumu ya Wizara Bungeni, jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi) akifafanua jambo wakati wa kikao kilichokuwakutanisha wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu pamoja na watendaji wa Wizara hiyo kujadili kuhusu Muundo na Majukumu ya Wizara Bungeni, jijini Dodoma.
Msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje, jiiji la Dodoma sehemu ya kwanza kipande cha Veyula-Mtumba-Ihumwa km 52.3, kwa kiwango cha lami, Eng. Tendai Kanda, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi,(Sekta ya Ujenzi), Eng Godfrey Kasekenya (kulia), kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo inayojengwa na kampuni ya China Civil Engineering Construction ltd.
Wanawake wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Uchukuzi) wakiwa katika maandamano kuadhimisha siku ya wanawake duniani yenye kauli mbiu "Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia Chachu katika kuleta Usawa wa Kijinsia", ambapo kwa upande wa mkoa wa Dodoma imefanyika wilayani Kondoa.
Watumishi wanawake wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, wakiwa katika maandamano walipoungana na wanawake duniani kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambapo mkoani Dodoma maadhimisho hayo yenye kauli mbiu "Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia Chachu katika kuleta Usawa wa Kijinsia" yamefanyika katika Wilaya ya Kondoa.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Bw. Saad Mtambule akimkabidhi Mkurugenzi wa Barabara toka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Eng. Alois Matei nyaraka za mkakati wa kudhibiti ajali kwa watumiaji wa barabara kwenye hafla ya kufunga mradi wa majaribio wa mpango wa hatua kumi (Ten step plan), wa miundombinu ya barabara salama nchini Tanzania. Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wataalamu mbalimbali wa miundombinu.
Muonekano wa jengo la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Arusha litakavyokuwa mara baaada ya kukamilika ujenzi wake. Jengo hilo linatarajiwa kuhudumia abiria laki sita kwa mwaka litakapokamilika.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, akikagua mlango wa kisasa wenye mfumo maalumu wa kitasa janja (Smart Lock) kwenye jengo la kitega uchumi la Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) mkoani Arusha. Vitasa hivyo vimefungwa mahsusi ili kuongeza mifumo ya ukusanyaji na udhibiti wa mapato.
Muonekano wa Jengo la Kitega Uchumi lenye ghorofa 10 linalojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa ajili ya makazi ya watumishi wa umma wa mkoa wa Arusha. Jengo hilo limekamilika kwa asilimia 98 na limegharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 5.5
Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Arusha, Eng. Reginald Massawe, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa pamoja na uongozi wa mkoa wakati wakikagua barabara ya Mianzini - Olemringa - Ngaramtoni Juu na Olemringaringa - Sambasha – Timbolo (Km 18) kwa kiwango cha lami ambao ujenzi wake umefikia asilimia 23, mkoani humo.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa wataalam wa Wakala wa Barabara nchini, TANROADS alipokagua maendeleo ya Ujenzi wa BRT III unaoanzia Posta ya zamani hadi Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu-Uchukuzi, Gabriel Migire ashiriki kwenye mdahalo katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji baina ya Tanzania na Umoja wa Ulaya, lililofanyika jijini Dar es Salaam, hivi karibuni.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya akiwa katika kikao cha 43 cha Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kilichofanyika jijini Burundi hivi karibuni. Ujumbe wa Mawaziri hao uliongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Katikati). Kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba.
Mkurugenzi Huduma za Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi) Mhandisi Aron Kisaka akizungumza na wadau wa kikao cha Maboresho ya Bandari (Hawapo pichani), wakati alipofungua kikao cha kwanza cha Wadau hao Mkoani Mtwara.
Title | Tarehe | Pakua |
---|---|---|
TANGAZO LA KOZI MAALUM YA MAOPARETA WA MITAMBO YA KAZI ZA UJENZI (GRADER OPERATOR COURSE) | 2022-11-09 | Pakua |